Classy Quote logo
  • Home
  • Categories
  • Authors
  • Topics
  • Who said

Mungu Quotes

Mungu quote from classy quote

Wanasayansi wanasema hakuna Mungu kwa sababu hawawezi kumwona wala kumgusa. Lakini nao hawana akili kwa sababu hawawezi kuiona wala kuigusa.

~ Enock Maregesi

Enock Maregesi Akili God Intelligence Mungu Scientists Wanasayansi

Usiingilie mambo ya mtu mwingine bila kibali kutoka kwa Mungu. Kuingilia mambo ya mtu mwingine bila kibali kutoka kwa Mungu ni dhambi. Dhambi hiyo itakuathiri. Hivyo, jali mambo yako – ya mwingine Mungu anayafanyia kazi – hadi utakapoitwa na Mungu kuingilia kati. Kuingilia kati mambo ya mtu mwingine kunaweza kuathiri mpango wa Mungu katika maisha yake. Hivyo, acha.

~ Enock Maregesi

Enock Maregesi Dhambi God God S Plan Kibali Life Maisha Mpango Wa Mungu Mungu Permission Sin

Wewe kuingilia mambo ya John ni sawa na kusema, ‘Mungu umeshindwa hebu ngoja na mimi nijaribu; ngoja niingilie kati kukusaidia juu ya maisha ya John Doe.’ Hiyo ni dhambi. Tena ni dhambi kubwa. Unajifananisha na Mungu; kwamba Mungu wa John Doe ameshindwa kwa hiyo mungu wewe ndiye utakayemtatulia matatizo yake. Amri kuu ya kwanza ya Mungu inasema, ‘Usiwe na miungu mingine ila mimi.’ Kuingilia mambo ya John tayari umevunja amri ya kwanza ya Mungu kwa kujifanya Mungu. Mungu ana mpango na maisha ya John, na anatumia matatizo yake kumfikisha kwenye takdiri aliyompangia. Hivyo, wewe si Mungu, acha Mungu afanye kazi yake. Mungu akikuruhusu kuingilia kati, yaani John akiamua kwa hiari yake mwenyewe kukuomba msaada wa mawazo au ushauri, maana yake ni kwamba Mungu amekuchagua wewe kuwa sehemu ya mafanikio ya John Doe.

~ Enock Maregesi

Enock Maregesi Dhambi God Help Life Maisha Mpango Msaada Mungu Plan Sin

Mungu ana uwezo wa kukuwekea ulinzi kulia na kushoto yaani anayekulinda naye ana mlinzi wake. Lakini wakati mwingine anaacha ufuate kile ambacho moyo wako unataka kwa sababu hataki kukulazimisha ijapokuwa uwezo huo anao. Mungu hakukuumba kuwa roboti. Alikuumba kuwa huru kuchagua mema au mabaya usije ukamlaumu baadaye kwamba ulimchagua yeye kwa sababu hukuwa na uhuru. Msikilize Roho wa Mungu, kabla na katika kila jambo unalofanya.

~ Enock Maregesi

Enock Maregesi Defence God Good Or Evil Heart Mema Au Mabaya Moyo Mungu Robot Roboti Ulinzi

Vita ya Shetani na Mungu inatuathiri zaidi sisi wanadamu – na hapo baadaye itamuathiri Shetani pia. Vita hii haiwezi kuisha hadi siku ya mwisho, Yesu Kristo atakaporudi kuwachukua wateule wake. Pambana kwa njia ya maombi hadi siku ya mwisho kwa sababu adui tunayepambana naye hana muda wa kupumzika. Pambana kujiombea na kuwaombea wengine waliohai, na hata wale ambao bado hawajazaliwa, kabla mafuta ya dunia hii hayajalipuka. Usiishi kama adui wa msalaba wa Yesu Kristo, badala yake, ishi kama rafiki wa msalaba wa Yesu Kristo. Kuishi kama rafiki wa msalaba wa Yesu Kristo ni kupinga majivuno yote ya Shetani kwa upendo uliotukuka wa kujishusha au kujidharirisha, kutokutetereka hata kidogo na tamaa za ulimwengu huu kwa upendo mkubwa wa umaskini, na kutokuyumba wakati wa matatizo kwa sababu wakati wa amani ulijilimbikizia imani.

~ Enock Maregesi

Enock Maregesi Adui Amani Battle Day Of Judgement Elects Enemy Faith Fight Friend God Humans Imani Jesus Christ Love Mafuta Ya Dunia Hii Majivuno Maombi Matatizo Msalaba Wa Yesu Kristo Mungu Needs Oil Of This World Pambana Peace Poverty Prayers Pride Rafiki Satan Shetani Siku Ya Mwisho Tamaa Za Ulimwengu Huu The Cross Of Jesus Christ The Desires Of This World Umaskini Upendo Vita Wanadamu Wateule Yesu Kristo

Kumwamini Mwenyezi Mungu wakati wa raha ni rahisi kuliko kumwamini Mwenyezi Mungu wakati wa shida, na utahitaji imani kuendelea kumwamini wakati wa dhiki. Vipindi vigumu katika maisha yetu hutokea kwa kila mmoja wetu. Kuamini ya kwamba Mungu ana makusudi ya lazima kukuondolea vikwazo katika maisha yako ni vigumu sana wakati mwingine, lakini imani ndicho kitu cha muhimu zaidi unachotakiwa kuwa nacho katika kipindi hiki ambacho dunia imekata tamaa. Amani ya Mungu, ambayo huzidi hekima na maarifa yote ya kibinadamu, ni kuliamini neno la Mungu kwamba ni la kweli. Bila imani hutaweza kumfurahisha Mungu. Imani ni ufunguo wa nguvu, uwezo na neema ambavyo Mungu ametupangia. Kwa ufupi, Mungu ni mkubwa kuliko wewe na matatizo yako.

~ Enock Maregesi

Enock Maregesi Ability Amani Ya Mungu Comfort Zone Deliberately Dhiki Difficulty Dunia Imekata Tamaa Faith God God Almighty Grace Imani Key Life Maisha Makusudi Matatizo Mungu Mwenyezi Mungu Neema Nguvu Obstacles Peace Of God Power Problems Ufunguo Uwezo Vikwazo Wakati Wa Raha World Has Given Up

Katika dunia ya leo ambapo mamilioni ya watu hutegemea utandawazi kupata pesa, kuwa na imani kwamba kupokea pesa kutoka kwa mtu usiyemjua au mtu mwenye nia mbaya na wewe ni kikwazo kikubwa cha maendeleo kwa sababu, karibu kila mtu unayekutana naye ni Shetani. Shetani ni mtu yoyote mwenye nia mbaya na wewe. Hivyo, kama uliwahi kuambiwa kwamba kupokea pesa kutoka kwa mtu usiyemjua ni kitu kibaya futa imani hiyo. Utaachaje kupokea pesa kutoka kwa mtu usiyemjua wakati kila siku unamwomba Mungu akusaidie, na Mungu hutenda kazi zake pale tunapojisahau? La sivyo hutapata pesa unayotamani kupata katika maisha yako, na kamwe hutawaamini watu. Zaka huondoa laana ya mapato. Toa zaka kununua pepo uliyopewa na Mungu.

~ Enock Maregesi

Enock Maregesi Curse Of Income Development Dunia Faith Globalization God Imani Laana Ya Mapato Life Maendeleo Maisha Malice Mamilioni Ya Watu Millions Of People Money Mtu Usiyemjua Mungu Nia Mbaya Paradise Pepo Pesa Satan Shetani Tithe Unanimous Person Utandawazi World Zaka
  • Classy Quote

    ClassyQuote has been providing 500000+ famous quotes from 40000+ popular authors to our worldwide community.

  • Other Pages

    • About Us
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    • Terms of Use
  • Our Products

    • Chrome Extention
    • Microsoft Edge Add-on
  • Follow Us

    • Facebook
    • Instagram
Copyright © 2025 ClassyQuote. All rights reserved.